1. |
H'a Mim
|
2. |
Naapa kwa Kitabu kinacho bainisha,
|
3. |
Hakika tumekiteremsha katika usiku ulio barikiwa. Hakika Sisi ni Waonyaji.
|
4. |
Katika usiku huu hubainishwa kila jambo la hikima,
|
5. |
Jambo litokalo kwetu. Hakika Sisi ndio wenye kutuma.
|
6. |
Ni rehema itokayo kwa Mola wako Mlezi. Hakika Yeye ni Mwenye kusikia Mwenye kujua.
|
7. |
Mola Mlezi wa mbingu na ardhi na vilio baina yao, ikiwa nyinyi mna yakini.
|
8. |
Hakuna mungu ila Yeye; anahuisha na anafisha- Mola Mlezi wenu na Mola Mlezi wa baba zenu wa mwanzo.
|
9. |
Lakini wao wanacheza katika shaka.
|
10. |
Basi ingoje siku ambayo mbingu zitakapo leta moshi ulio dhaahiri,
|
11. |
Utakao wafunika watu: Hii ni adhabu chungu!
|
12. |
Mola wetu Mlezi! Tuondolee adhabu hii. Hakika tutaamini.
|
13. |
Nini faida ya kukumbuka kwao? Na alikwisha wafikia Mtume mwenye kubainisha.
|
14. |
Na wao wakamgeuzia uso, na wakasema: Huyu amefunzwa, naye ni mwendawazimu.
|
15. |
Hakika sisi tutaiondoa adhabu kidogo, lakini nyinyi kwa yakini mtarejea vile vile!
|
16. |
Siku tutayo yashambulia mashambulio makubwa, bila ya shaka Sisi ni wenye kutesa.
|
17. |
Na hakika kabla ya hawa tuliwafanyia mtihani watu wa Firauni, na aliwafikia Mtume Mtukufu.
|
18. |
Akasema: Nipeni waja wa Mwenyezi Mungu; kwa hakika mimi kwenu ni Mtume Muaminifu.
|
19. |
Na msimfanyie kiburi Mwenyezi Mungu; hakika mimi nitakuleteeni uthibitisho ulio wazi.
|
20. |
Nami najikinga kwa Mola wangu Mlezi na ndiye Mola wenu Mlezi pia, ili msinipige mawe.
|
21. |
Na ikiwa hamniamini, basi jitengeni nami.
|
22. |
Ndipo akamwomba Mola wake Mlezi: Hakika watu hawa ni wakosefu.
|
23. |
Mwenyezi Mungu akasema: Basi nenda na waja wangu usiku. Kwa yakini mtafuatwa.
|
24. |
Na iache bahari vivyo hivyo imeachana, hakika wao hao ni jeshi litakalo zamishwa.
|
25. |
Mabustani mangapi, na chemchem ngapi waliziacha!
|
26. |
Na mimea na vyeo vitukufu!
|
27. |
Na neema walizo kuwa wakijistareheshea!
|
28. |
Ndio hivyo! Na tukawarithisha haya watu wenginewe.
|
29. |
La mbingu wala ardhi hazikuwalilia, wala hawakupewa muhula.
|
30. |
Na bila ya shaka tuliwaokoa Wana wa Israili katika adhabu ya kuwadhalilisha,
|
31. |
Ya Firauni. Hakika yeye alikuwa jeuri katika wenye kupindukia mipaka.
|
32. |
Na tuliwakhiari kwa ujuzi wetu kuliko walimwengu wenginewe.
|
33. |
Na tukawapa katika ishara zenye majaribio yaliyo wazi.
|
34. |
Hakika hawa wanasema:
|
35. |
Hapana ila kufa kwetu mara ya kwanza tu, wala sisi hatufufuliwi.
|
36. |
Basi warudisheni baba zetu, ikiwa nyinyi mnasema kweli.
|
37. |
Je! Ni wao bora au watu wa Tubbaa' na walio kuwa kabla yao? Tuliwaangamiza. Hakika hao walikuwa wakosefu.
|
38. |
Na hatukuziumba mbingu na ardhi na vilivyomo baina yake kwa mchezo.
|
39. |
Hatukuviumba hivyo ila kwa Haki, lakini wengi wao hawajui.
|
40. |
Hakika siku ya Uamuzi ni wakati ulio wekwa kwa wao wote.
|
41. |
Siku ambayo rafiki hatamfaa rafiki yake kwa chochote, wala hawatanusuriwa.
|
42. |
Isipo kuwa atakaye mrehemu Mwenyezi Mungu. Hakika Yeye ndiye Mwenye nguvu, Mwenye kurehemu.
|
43. |
Hakika Mti wa Zaqqum,
|
44. |
Ni chakula cha mwenye dhambi.
|
45. |
Kama shaba iliyo yayushwa, hutokota matumboni
|
46. |
Kama kutokota kwa maji ya moto.
|
47. |
(Itasemwa:) Mkamateni na mtupeni katikati ya Jahannamu!
|
48. |
Kisha mmwagieni juu ya kichwa chake adhabu ya maji yanayo chemka.
|
49. |
Onja! Ati wewe ndiye mwenye nguvu, mtukufu!
|
50. |
Hakika haya ndiyo mliyo kuwa mkiyatilia shaka.
|
51. |
Hakika wachamngu watakuwa katika mahali pa amani,
|
52. |
Katika mabustani na chemchem,
|
53. |
Watavaa hariri nyepesi na hariri nzito wakikabiliana,
|
54. |
Hivi ndivyo itakavyo kuwa, na tutawaoza mahurilaini.
|
55. |
Humo watataka kila aina ya matunda, na wakae kwa amani.
|
56. |
Humo hawataonja mauti ila mauti yale ya kwanza, na (Mwenyezi Mungu) atawalinda na adhabu ya Jahannamu,
|
57. |
Kuwa ni fadhila zitokazo kwa Mola wako Mlezi. Huko ndiko kufuzu kukubwa.
|
58. |
Basi tumeifanya nyepesi hii Qur'ani kwa ulimi wako, ili wapate kukumbuka.
|
59. |
Ngoja tu, na wao wangoje pia.
|