1. |
Muulizaji aliuliza juu ya adhabu itakayo tokea,
|
2. |
Kwa makafiri - ambayo hapana awezaye kuizuia -
|
3. |
Kutoka kwa Mwenyezi Mungu Mwenye mbingu za daraja.
|
4. |
Malaika na Roho hupanda kwendea kwake katika siku ambayo kadiri yake ni miaka khamsini elfu!
|
5. |
Basi subiri kwa subira njema.
|
6. |
Hakika wao wanaiona iko mbali,
|
7. |
Na Sisi tunaiona iko karibu.
|
8. |
Siku ambayo mbingu zitakapo kuwa kama maadeni iliyo yayushwa.
|
9. |
Na milima itakuwa kama sufi.
|
10. |
Wala jamaa hatamuuliza jamaa yake.
|
11. |
Ijapo kuwa wataonyeshwa waonane. Atatamani mkosefu lau ajikomboe na adhabu ya siku hiyo kwa kuwatoa fidia wanawe,
|
12. |
Na mkewe, na nduguye,
|
13. |
Na jamaa zake walio kuwa wakimkimu,
|
14. |
Na wote waliomo duniani, kisha aokoke yeye.
|
15. |
La, hasha! Kwa hakika huo ni Moto mkali kabisa,
|
16. |
Unao babua ngozi ya kichwa!
|
17. |
Utamwita kila aliye geuza mgongo na akageuka.
|
18. |
Na akakusanya mali, kisha akayahifadhi.
|
19. |
Hakika mtu ameumbwa na papara.
|
20. |
Inapo mgusa shari hupapatika.
|
21. |
Na inapo mgusa kheri huizuilia.
|
22. |
Isipo kuwa wanao sali,
|
23. |
Ambao wanadumisha Sala zao,
|
24. |
Na ambao katika mali yao iko haki maalumu
|
25. |
Kwa mwenye kuomba na anaye jizuilia kuomba;
|
26. |
Na ambao wanaisadiki Siku ya Malipo,
|
27. |
Na ambao wanaiogopa adhabu itokayo kwa Mola wao Mlezi.
|
28. |
Hakika adhabu ya Mola wao Mlezi si ya kuaminika nayo.
|
29. |
Na ambao wanahifadhi tupu zao.
|
30. |
Isipo kuwa kwa wake zao, au iliyo wamiliki mikono yao ya kuume, basi hao hawalaumiwi -
|
31. |
Lakini wanao taka kinyume ya haya, basi hao ndio wanao ruka mipaka.
|
32. |
Na ambao wanazichunga amana zao na ahadi zao,
|
33. |
Na ambao wanasimama imara katika ushahidi wao,
|
34. |
Na ambao wanazihifadhi Sala zao.
|
35. |
Hao ndio watakao hishimiwa Peponi.
|
36. |
Wana nini wale walio kufuru wanakutumbulia macho tu?
|
37. |
Makundi kwa makundi upande wa kulia na upande wa kushoto!
|
38. |
Kwani kila mmoja wao anatumai kuingizwa katika Pepo ya neema?
|
39. |
La, hasha! Hakika Sisi tumewaumba kutokana na wanacho kijua.
|
40. |
Basi naapa kwa Mola Mlezi wa mashariki zote na magharibi zote kwamba Sisi tunaweza
|
41. |
Kuwabadili kwa walio bora kuliko wao; na Sisi hatushindwi.
|
42. |
Basi waache wapige porojo na wacheze, mpaka wakutane na siku yao wanayo ahidiwa,
|
43. |
Siku watakapotoka makaburini kwa upesi kama kwamba wanakimbilia mfundo,
|
44. |
Macho yao yatainama, fedheha itawafunika. Hiyo ndiyo Siku waliyo kuwa wakiahidiwa.
|