Meal Seç / Sure Seç

AL - QAARIA'H Suresi

(SWAHILI) QURAN


101 - AL - QAARIA'H
KWA JINA LA MWENYEZI MUNGU MWINGI WA REHEMA MWENYE KUREHEMU.
        
1. Inayo gonga!
2. Nini Inayo gonga?
3. Na nini kitacho kujuilisha nini Inayo gonga?
4. Siku ambayo watu watakuwa kama nondo walio tawanyika;
5. Na milima itakuwa kama sufi zilizo chambuliwa!
6. Basi yule ambaye mizani yake itakuwa nzito,
7. Huyo atakuwa katika maisha ya kupendeza.
8. Na yule ambaye mizani yake itakuwa khafifu,
9. Huyo maskani yake yatakuwa Moto wa Hawiya!
10. Na nini kitacho kujuilisha nini hiyo?
11. Ni Moto mkali!
KURAN uygulamasını telefonunuza siz de yükleyin: